Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa akipanda mti katika Bustani ya Tasafu Ndembezi.
Mwenyekiti
wa Chama Chamapinduzi (CCM )Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa amewataka wananchi kumpongeza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa
kuendelea kuleta fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mkoa wa
Shinyanga Ikiwa ni sehemu ya kuungamkoano jitihada zake.
Mabala
amesema hayo leo Juni 25, 2023 katika viwanja vya bustani ya TASAF (zamani soko
la mirunda) Kata ya Ndembezi, Manispaa ya Shinyanga wakati wa mkutano wa
hadhara alio fanya katika kata hiyo ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha ziara yake
ya siku saba aliyofanya kwa lengo la kuimarisha chama, na kukagua utekelezaji
wa ilani ya Chama Chamapinduzi mkoani humo ya mwaka 2020 – 2025 ikiwa ni pamoja
na kusikilizaji na kutatua kero zinazo wakabili wananchi wa Wilaya ya Shinyanga
Mjini.
Mabala Pia amempongeza Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Mhe. Patrobas Katambi pamoja na
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kuongeza ukusanyaji
wa mapato na kuvuka lengo la bajeti sambamba na kusimamia vizuri matumizi ya fedha za miradi
ya maendeleo zinazo tolewa na serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Dkt.
Samia Suluhu Hassan.
"Nampongeza
Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya na sasa Mkoa wetu unang'aa
kila mahali kutokana na fedha nyingi za maendeleo zilizo letwa na serikali kwa
ajili ya utekelezaji wamiradi mbalimbalimbali ikiwemo sekta ya Afya ,Maji,Nishati,Miundo
mbinu na Elimu ,mesema Mabala.
Aidha Mabala amewataka wananchi wa Manispaa ya Shinyanga na mkoakwa ujumla kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi huku akiitaja baadhi ya miradi iliyo tekelezwa kuwa ni pamoja na Soko la kisasa, soko la mitumba na soko la wajasiriamali.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa
Shinyanga Mabala Mlolwa akiongozana na Viongozi wachama hicho wilaya na mkoa.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa
Shinyanga Mabala Mlolwa akiongozana na Viongozi wachama hicho wilaya na mkoa.
Wananchi wakiwa kwenye mkutano uliohitishwa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Shinyanga mjini Makombe akimkaribisha mwenyekiti wa CCM mkoa Mabala Mlolwa .
Wakuu waidara na vitengo wakisubiri kujibu hoja kwenye mkutano.
0 Comments