6/recent/ticker-posts

CHEMSHA BONGO NA SALOME MAKAMBA YAWAPA FURAHA WASIKILIZAJI WA REDIO FARAJA SHINYANGA


Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inayoendeshwa na Kituo cha Matangazo Redio Faraja Fm Stereo kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba wamekabidhiwa zawadi mbalimbali ikiwemo Majiko ya Gesi, Jezi na Mipira, Madaftari, taulo za kike pamoja Fedha kwa ajili ya kuviongezea mtaji wa bila riba wala marejesho vikundi mbalimbali vikiwemo vya wanawake, vijana, wazee na wenye ulemavu.

Hafla fupi ya makabidhiano ya zawadi hizo imefanyika leo Jumatatu Septemba 11,2023 katika viwanja vya Redio Faraja Mjini Shinyanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali na wawakilishi wa makundi ya kijamii.

Akizungumza wakati kukabidhi zawadi kwa washindi, Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba amewapongeza washindi wote na kuahidi kuwa Chemsha Bongo na Salome ni zoezi endelevu.

"Nawapongeza sana wafanyakazi wa Redio Faraja kwa kuendesha zoezi hili kwa weledi mkubwa. Mimi ni mwanasiasa lakini hili Jambo tunalolifanya hapa tunalofanya kwa kushirikiana na Radio Faraja siyo la kisiasa bali ni la kusaidia jamii. Tunapenda kuwezesha makundi mbalimbali ya wananchi wakiwemo watu wenye ulemavu, wanafunzi, vijana na wanawake. Maswali yanayoulizwa yanatujenga na kutuunganisha wana Shinyanga",amesema Makamba.

"Naomba zoezi hili liwe chachu kwa wadau wengine kusaidia makundi ya watu katika jamii. Tunataka kukuza uchumi, kutokomeza ukatili na kulinda mazingira kwa kutumia nishati mbadala ndiyo maana mmeshuhudia tukigawa pia majiko ya gesi kwa ajili ya kutunza mazingira",amesema.

Mratibu wa Chemsha Bongo na Salome Makamba, Simeo Makoba amesema Washindi hao, wamepatikana baada ya kujibu kwa usahihi maswali yaliyokuwa yakiulizwa kupitia vipindi mbalimbali vya Redio Faraja Fm Stereo ambayo yanaandaliwa kwa lengo la kuibua vipaji na kuwapa wananchi msukumo wa kutafuta taarifa kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kufuatilia na kujua mipango ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

"Tumekuwa tukiendesha Chemsha Bongo na Salome Makamba tangu mwezi uliopita na Washindi wanaopatikana wanatoka katika makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo watu wenye ulemavu, wazee, vijana, wanawake na wanafunzi. Ili kushiriki Chemsha Bongo na Salome Makamba inakubidi ujibu kwa usahihi maswali yanayoulizwa na waendeshaji wa vipindi kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii",amesema Makoba.

"Chemsha Bongo na Salome Makamba hufanyika kupitia kipindi cha Michapo ya jioni kinachofanyika Jumatatu hadi Alhamisi kuanzia saa 10:15 hadi saa 11:00 jioni, kipindi cha Dimbanileo kinachofanyika kila siku kuanzia saa 2:00 hadi saa 3:00 usiku, na kwa makundi maalum ya wanawake, vijana, wazee na wenye ulemavu kila Ijumaa kuanzia saa 3:00 hadi saa 3:30 usiku. Kwa upande wa wanafunzi Chemsha bongo na Salome Makamba inafanyika kila Jumamosi kuanzia saa 4:15 hadi saa 4:30 asubuhi",amesema Makoba.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, John Tesha akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga amempongeza Mbunge Salome kwa ubunifu huo ambao unachangamsha jamii na kusaidia jamii.

Mkurugenzi Msaidizi wa Redio Faraja Anikazi Kumbemba amesema zoezi hilo linaendeshwa kwa uwazi mkubwa kupitia Redio hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki.

Nao washindi waliopata zawadi wamemshukuru Mbunge Salome Makamba kwa ubunifu huo huku wakiahidi kuwa wasikilizaji wazuri wa vipindi vinavyorushwa Redio Faraja.

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba akizungumza leo Jumatatu Septemba 11,2023 wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge huyo wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba.


Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi ya shilingi 300,000/= kwa Wapiga picha Mjini Shinyanga ambao ni washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba.

Mwakilishi wa Shirika la Haki Yangu Foundation, John Eddy akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba. 
Mkuu wa Dawati la Jinsia Mkoa wa Shinyanga SSP Monica Sehere ambaye ni Polisi Jamii Mkoa wa Shinyanga  akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba. 
Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, John Tesha  akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba. 


Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba . 
Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi jiko la Gesi kwa mmoja wa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba. 

Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .
Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .

Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .

Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .

Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .
Wadau na Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba wakifuatilia matukio wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba
Wadau na Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba wakifuatilia matukio wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba ambayo inaendeshwa na Redio Faraja kwa kushirikiana na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga Salome Makamba
Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .

Mbunge wa Viti Maaalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Salome Makamba (aliyevaa tisheti nyeupe) akikabidhi zawadi kwa washindi wa awamu ya pili ya Chemsha bongo na Salome Makamba .

Post a Comment

0 Comments