Programu
hiyo inatekelezwa katika Mikoa 26 ya Tanzania bara ambapo uzinduzi kwa ngazi ya
Taifa ulifanyika Desemba 13,2021 ambapo ilizinduliwa na Waziri wa maendeleo ya
jamii, jinsia, wanawake na makundi maaluma Dkt. Dorothy Gwajima kwa niaba ya
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akizindua
programu hiyo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, mkuu wa Wilaya ya Kishapu
Joseph Mkude amewaagiza waratibu wa PJT – MMMAM kufanyakazi kwa ubunifu na
kuandaa mpango kazi unaogusa maeneo yote ya kimkakati ikiwemo kuzifikia sekta
za umma na sekta binafsi.
DC
Mkude amewaomba wadau na watu wote watakaoshiriki kwenye PJT – MMMAM
kuhakikisha wanatoa kipaumbele na kuweka mipango ya utekelezaji wa maeneo hayo
kuanzia ngazi ya familia na maeneo ya kazi.
“Nawaagiza
waratibu kufanyakazi kama timu ya ushindi kwa kuandaa mpango kazi unaogusa
maeneo yote ya kimkakati na kuzifikia sekta za umma na sekta binafsi lengo ni
kuwapa fursa waajiri na watumishi wao ili kuhakikisha wanatoa fursa na
kipaumbele katika malezi, makuzi na malezi ya awali ya mtoto wakati wawapo
kazini na nyumbani”.amesema DC Mkude
Awali
akizungumza afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Shinyanga Bwana Tedson Ngwale
amesema utekelezaji wa programu jumuishi ya Taifa ya makuzi na malezi ya awali
ya mtoto (PJT – MMMAM) umelenga maeneo makuu matano (5) ya kimkakati ambayo ni
pamoja na upatikanaji wa Afya bora kwa mtoto, lishe bora kwa mtoto, malezi ya
mwitikio, usalama na ulizi wa mtoto pamoja na fursa za ujifunzaji wa awali.
Kwa
upande wake mwakilishi kutoka shirika la ICS Sabrina Majikata amesema PJT –
MMMAM imelenga kuwaimarisha watoto kuanzia umri 0 hadi miaka nane (8) ambapo
amesema ni jukumu la kila mtu kuwalinda watoto wa kike na watoto wa kiume ili
waweze kukua na kufikia utimilifu wao.
Baadhi
ya viongozi wa serikali na wadau akiwemo katibu wa kampeni ya kupinga ukatili
inayoitwa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Mkoa wa
Shinyanga, Bwana Daniel Kapaya amesema programu PJT – MMMAM itasaidia
kupunguza ukatili unaoendelea katika jamii.
Programu
jumuishi ya Taifa ya makuzi na malezi ya awali ya mtoto (PJT – MMMAM)
imezinduliwa leo Jumatano Septemba 20,2023 Mkoani Shinyanga na kuhudhuriwa na
viongozi wa serikali, taasisi binafsi pamoja na wadau mbalimbali.
0 Comments