6/recent/ticker-posts

Picha :JESHI LA POLISI MKOA WA SHINYANGA LAZINDUA RASMI KAMPENI YA "TUWAAMBIE KABLA HAWAJAHARIBIWA" , WADAU WAPONGEZA UBUNIFU WAJESHI LA POLISI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga leo Oktoba 18, 2024 limezindua kampeni ya "Tuwaambie kabla hawajaharibiwa" yenye lengo la kufikisha ujumbe kwa wanafunzi wote wa Shule za msingi, Sekondari na vyuo vya kati mkoani humo.

Kampeni hiyo imezinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude ambaye amemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha katika kuzindua Kampeni hiyo, ambapo amelipongeza Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha dawati la Jinsia na watoto kwa kubuni na kuzindua kampeni hiyo yenye lengo la kuwajengea uwezo watoto na vijana kuweza kutambua hatari na kuchukua tahadhari ili wasijiunge katika makundi ambayo yanaweza kupelekea kutofikia ndoto zao.

Aidha Mhe. Mkude amewakumbusha wazazi na walezi kuwa mtoto hajawahi kukua kwa mzazi wake hivyo wasichoke kuwafundisha na kuwakemea pale ambapo wanaenda kinyume na maadili ya nchi yetu.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Polisi Jamii mkoani humo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Fraterine Tesha amesema kuwa kampeni hiyo ni maalum kwa ajili ya kuwajengea uelewa watoto pamoja na vijana wa Shule za msingi, Sekondari na vyuo vya kati.
  
  "Napenda kumshukuru Afande Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania kwa kuruhusu kampeni hii kutekelezwa nchi mzima ambayo kitaifa ilizinduliwa rasmi Agosti 29, 2024 mkoani Njombe hii itasaidia kuwatayarisha vijana wetu ili kujenga Taifa la kizazi chenye maadili mema" alisema ACP - Tesha.

Naye afisa ustawi wa Jamii Halmashauri ya Kishapu ndugu Paul Palaso amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kampeni hiyo ambayo itaokoa jamii kutokana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto,  "tumewahi kuona madhara mengi sana ya ukatili wa kimwili ambao unapelekea vifo na ulemavu wa kudumu kwa watoto wetu pia ukatili unadumaza Taifa hivyo tutumie vyema kampeni hii kuongea na watoto wetu kuwaelimisha na kuwafuatilia kwa ukaribu mienendo yao ili wasije wakaharibiwa.
Msanii Nyumbu Mjanja akiwa nabango lenye ujumbe kwenye maandamano ya uzinduzi wa kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Polisi Jamii mkoani humo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Fraterine Tesha akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akiwa na mwakilishi wa Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Shinyanga Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Fraterine Tesha wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa Kishapu.
Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Kishapu (OCD) Esther Zephania Gesogwe akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa Kishapu.
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akiwa na mwakilishi wa Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Shinyanga Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Fraterine Tesha wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa Kishapu.
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akiwa na mwakilishi wa Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga akiwa na Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Shinyanga Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP)  Fraterine Tesha pamoja na OCD Wiliaya ya Kishapu Esther Zephania Gesogwe
Askari Polisi na wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.


Meneja wa Benki ya NMB Tawi wilaya ya Kishapu akiwasalimia wageni wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi pamoja na Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi na wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi na wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari Polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Msanii Nyumbu Mjanja akitoa burudani ya wimbo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Msanii Nyumbu Mjanja akitoa burudani ya wimbo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Wadau pamoja na Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi pamoja na Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi pamoja na Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.

Askari polisi pamoja na Wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi pamoja na Wanafunzi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.
Askari polisi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.







Mabango mbalimbali wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Tuwaambiea kabla hawajaharibiwa.









Post a Comment

0 Comments