6/recent/ticker-posts

RC MNDEME AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI ULIO TEKELEZWA NA SHIRIKA LA LIFEWATER INTERNATIONAL KWA KUSHIRIKIANA NA RUWASA SHINYANGA

Mhe.Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme akizindua mradi wamaji wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.058 Mwalukwa.
Na.Amo Blog Shinyanga

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme amezindua mradi wamaji wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.058 unaotekelezwa na Shirika la Lifewater International kwa kushirikiana na Wakala wamaji na Usafi wamazingira Vijijini (RUWASA)Wilaya ya Shinyanga .

Akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi huo,Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme  amelipongeza Shirika la Lifewater International , kwa kutekeleza mradi wa maji ndani ya mkoa wa Shinyanga ambao umetekelezwa kwenye kata ya Mwalukwa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga hali itakayo saidia kuwaondolea wananchi changamoto ya kutumia maji yasiyo kuwa safi na salama pamoja na kutembea umbali mrefu wakitafta huduma ya maji.

 Mhe.Mndeme amesema Serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  inasisitiza sana upatikanaji wa maji karibu na makazi ya wananchi ili kufikia adhima ya Dkt.Samia ya kumtua mama ndoo kichwani na kuondokana na adha ya ukosefu wa maji safi na salama, pamoja na kuugua magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji ambayo siyo salama kiafya.

“Tunalishukuru sana Shirika hili la Lifewater International kwa kutekeleza mradi huu wa maji Ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ,  ambapo tunaomba mradi huu pia ufike na kwenye maeneo mengine ambayo yana shida ya maji safi na salama,”amesema Mndeme.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Lifewater International Tanzania Devocatus Kamara, amesema mradi huo umetekelezwa kwenye kata ya Mwalukwa halmshauri ya wilaya ya Shinyanga kwa kiasi cha Shilingi za kitanzania bilioni 1.058 huku akieleza kuwa mradi huo unatarajia kukamilika Mwezi March mwaka 2024.

 Kwa upande wao baadhi ya Wananchi wa Kata ya Mwalukwa wameishukuru serikali pamoja na Shirika la Lifewater International kwa kuwajengea mradi wa maji katika kata hiyo mradi utakao saidia kupunguza adha ya kutembea umbali mrefu wakitafta huduma ya maji na kuondokana na changamoto ya kutumia maji yasiyo kuwa safi na salama.












Post a Comment

0 Comments