Akiongoza mahafari hayo mgeni rasmi ambaye
ni katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo
ameupongeza uongozi wa kituo hicho kwa kuboresha mazingira ya kulelea watoto na
kuwaomba wazazi na walezi kupeleka watoto wao katika kituo hicho kwani kituo
kinawalea watoto katika maadili na kuwajengea uwezo wakufanya vizuri kitaaluma.
Kwa upande wake mkurugenzi wa kituo hicho
Damary Mollessi akitoa taarifa ya kituo hicho amesema kuwa kituo kunapokea na
kutoa malezi kwa watoto wa kuanzia mwaka mmoja hadi miaka mitano na kuwalea
watoto hao katika maadili na kuhakikisha watoto wanao hitimu katika kituo hicho
wanafanya vizuri kitaaluma.
Pia Damary amewaomba wazazi na walezi kupeleka watoto wao wenye umri wa mwaka mmoja hadi miaka mi tano katika kituo hicho kilichopo karibu na ofisi za mabasi ya Okasi mwasele maana kituo hicho kinatoa malezi na elimu bora kwa watoto.
Damary ameeleza kuwa Kituo cha Angel Gabriel kimesajiliwa kwa usajili wa namba 2726 ambapo amewaomba wazazi wanao hitaji fomu kwa ajili ya watoto kujiunga na kituo hicho kutembelea kituoni au kupiga sumu kwa mkurugenzi wa kituo kwa simu na 0752516753/0675969213.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza na wazazi na walezi wawatoto wanao lelewa katika kituo cha Angel Gabriel Day Care Center Mwasele Manispaa ya Shinyanga
watoto wanao lelewa na kufundishwa katika kituo cha Angel Gabriel day care wakionyesha vipaji vyao
Watoto wanao lelewa na kufundishwa katika kituo cha Angel Gabriel day care wakionyesha vipaji vyao
Mkurugenzi wa kituo cha Angel Gabriel Damary Mollessi akitoa taarifa ya kituo kwa mgeni rasmi.
Watoto wanao lelewa na kufundishwa katika kituo cha Angel Gabriel day care wakionyesha vipaji vyao.
0 Comments