6/recent/ticker-posts

TAASISI YA NASIMAMA NA MAMA MKOA WA SHINYANGA WAMPA MITANO DKT.SAMIA,WAWEKA MKAKATI WAKUPAMBANA NA UKATILI

Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wakanda katika picha ya pamoja baada ya kikao.

Na Mwandishi wetu Amo blog  Shinyanga.
Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga Umempongeza Rais Samia Suluhu Hassan na Kutoa Ahadi ya Kumunga Mkono Katika Uchaguzi Mkuu

Leo, April 6, 2025, uongozi wa Taasisi ya Nasimama na Mama Popote Nilipo Mkoa wa Shinyanga ukiongozwa na mwenyekiti wa taasisi hiyo mkoa wa Shinyanga Bi.Zamda Shabani pamoja na katibu wa Taasisi Bi.Tatu Almas umefanya kikao cha kipekee kilichofanyika katika eneo la Mazingira Senta, Manispaa ya Shinyanga kwa lengo la viongozi wamkoa kutaka kufahamiana na kupanga mikakati ya kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu ujao.

Viongozi wa taasisi hiyo wametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Samia kwa uongozi wake imara na juhudi zake za kuleta maendeleo nchini.

Katika mkutano huo, viongozi wa taasisi hiyo wameelezea jinsi Rais Samia alivyokuwa na mchango mkubwa katika kuboresha sekta mbalimbali za kiuchumi, kijamii, na kisiasa, huku wakisisitiza kuwa ni muhimu kumuunga mkono ili kuendeleza mafanikio hayo.

Aidha viongozi hao wamebainisha kuwa Rais Samia ni kiongozi ambaye ameonyesha uwezo wa kuleta mabadiliko na maendeleo endelevu, hivyo wanajukumu la kuhakikisha anapata sapoti kubwa kutoka kwa wananchi, hasa katika mkoa wa Shinyanga katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Katika kikao hicho, viongozi wa taasisi ya Nasimama na Mama wamejadili na kupanga mikakati ya kuhamasisha wananchi kuendelea kumuunga mkono Rais Samia, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha anapata ushindi mkubwa.

Pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Nasimama na Mama Popote Nilipo Kanda ya Serengeti, Osca Kaijage, pamoja na Katibu wa Kanda ya Serengeti, Bw. Renatus Nzemo, wamehudhuria kikao hicho na kutoa michango muhimu.

 Kaijage amesisitiza umuhimu wa viongozi wa taasisi kushirikiana kwa karibu na jamii, na kumsaidia Rais Samia kupata ushindi kwa kishindo katika uchaguzi mkuuu

Pamoja na kujadili masuala ya kisiasa, kikao hicho pia kimejadili masuala ya kijamii, hasa mapambano dhidi ya ukatili ambapo Wanachama wa taasisi wameonyesha dhamira ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika kupambana na ukatili, kwa lengo la kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na usalama na ustawi iwapo wataungana kukemea vitendo vya ukatili, hasa kwa wanawake na watoto.

Katika mjadala huo, wameeleza kuwa ni muhimu kuwafikia watu wengi kwa kutoa elimu ya madhara ya ukatili na jinsi ya kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji.

Katika kumalizia kikao hicho, wanachama wa taasisi wameeleza dhamira yao ya kuendelea kushirikiana na Serikali ya Rais Samia katika kutokomeza vitendo vya ukatili na kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na mazingira salama huku wakisisitiza kuwa ni muhimu kuwa na mfumo imara wa kutoa msaada kwa wahanga wa ukatili, pamoja na kuongeza uhamasishaji kwa jamii kuhusu umuhimu wa haki na usawa kwa wote.

Kwa kumalizia, wanachama wa taasisi hiyo walionesha wazi kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali ya Rais Samia ili kuleta mabadiliko ya kudumu katika kupambana na ukatili, huku wakiwa na lengo la kuhakikisha kuwa jamii inaishi katika mazingira yenye amani, usawa, na haki.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Nasimama na Mama Popote Nilipo Kanda ya Serengeti, Osca Kaijage,akizungumza na viongozi wa taasisi ya Nasimama na mama mkoa wa Shinyanga.Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wakanda katika picha ya pamoja baada ya kikao.Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wakanda katika picha ya pamoja baada ya kikao.Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wakanda katika picha ya pamoja baada ya kikao.Katibu wa Taasisi ya Nasimama na mama Kanda ya Serengeti, Bw. Renatus Nzemo, akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Nasimama na mama mkoa wa Shinyanga. Katibu wa Taasisi ya Nasimama na mama Kanda ya Serengeti, Bw. Renatus Nzemo, akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Nasimama na mama mkoa wa Shinyanga. 

Mwenyekiti wa Taasisi ya Nasimama na Mama Popote Nilipo Kanda ya Serengeti, Osca Kaijage,akizungumza na viongozi wa taasisi ya Nasimama na mama mkoa wa Shinyanga.
Uongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wakanda katika picha ya pamoja baada ya kikao.
Kikao cha ongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga kikiendelea.
Kikao cha ongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga kikiendelea.

Kikao cha ongozi wa Taasisi ya "Nasimama na Mama Popote Nilipo" Mkoa wa Shinyanga kikiendelea.

Post a Comment

0 Comments