Uongozi wa Mkoa wa
Shinyanga unatarajia kufanya uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya Msaada wa
Kisheria ya Mama Samia (MAMA SAMIA Legal Aid Campaign) Uzinduzi unaotarajia kufanyika katika uwanja wa Sabasaba
Halmashuri ya Manispaa ya Shinyanga mkoani humo.
Akizungumzia maandalizi
ya kampeni hiyo Msajili wa Watoa huduma ya Msaada wa Kisheria mkoa Tedson Ngwale amesemakuwa maandalizi ya uzinduzi wa kampeni hiyo
yanaendelea kufanyika ili kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa kwa ufanisi na
kuleta tija kwa wananchi .
Aidha Ngwale amewaomba
wananchi wa mkoa wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa sabasaba ili waweze kujifunza mambo mbalimbali juu upatikanaji wa huduma ya msaada wa kisheria.
0 Comments