Kuelekea kipindi cha mwishoni
mwa mwaka jshi la polisi mkoani Shinyanga limejipanga kuimarisha usalama na
kuzuia maandamano na mikusanyiko inayoashiria vurugu ndani ya mkoa wa
Shinyanga.
Akizungumza
mara baada ya zoezi hilo lililoambatana na matembezi ya mataa kwa mataa Kamanda
wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP. Janeth Magomi amebainisha kuwa jeshi la polisi
limejipanga kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao na kupiga marufuku
maandamano na mikusanyiko inayoashiria vurugu.
"Tumejipanga
madhubuti kuhakikisha kuwa tunapo kwenda mwisho wa mwaka tunasimamia jukumu
letu la msingi la kulinda usalama wa raia na mali zao, uharifu wa mwisho wa
mwaka ikiwemo unyang'anyi wa kutumia nguvu na siraha tutakabiliana nayo na
kusimamia usalama", amesema Kamanda Magomi.
Aidha
Kamanda Magomi amewataka watumiaji wa vyomba vya usafiri kufuata sheria na
taratibu za usalama barabarani lakini pia amepiga marufuku maandamano,
mikusanyiko inayoashiria vurugu ndani ya Shinyanga.
"Lakini
pia maandamano na mikusanyiko ya aina yoyote inayoashiria vurugu ndani ya
Shinyanga vyote tunavikataza na ni marufuku hivyo niwahakikishie watu wa
Shinyanga tumejipanga vikosi vyote kuhakikisha tunalinda usalama wa raia na
mali zao", aliongeza Kamanda Magomi.
0 Comments