Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme akiwa katika kikao kazi na
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji
Na Amo Blog Shinyanga
MKUU wa mkoa wa shinyanga Mhe. Christina S.
Mndeme amefanya kikao kazi na Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji
kwa lengo la kuwakumbusha majukumu yao ya kazi ikiwemo kusimamia utekelezaji wa
miradi ya maendeleo, utatuzi wa kero za wananchi, kuongeza kasi ya ukusanyaji
mapato, kueleza umma juu ya fedha wanazopokea kutoka serikali kuu, utunzaji wa
mazingira na kupambana dhidi ya ukatili wa kijinsia katika maeneo yao.
Mhe. Mndeme ameyasema hayo leo tarehe 10
Oktoba, 2023 wakati alipokutana na wataalam hao katika ukumbi wa mikutano
uliopo shule ya savannah plains huku akiwasisitiza kwenda kuzingatia maadili na
nidhamu huku akikemea tabia ya kuchati na simu wanapokuwa wakiwahudumia
wananchi huku akisisitiza kuwa kipaumbele cha serikali ni utoaji wa huduma bora
kwa wananchi wenyewe na ndiyo maelekezo ya Mhe. Rais.
"Nendeni mkasimamie utekelezaji wa miradi
ya maendeleo, mkatoe elimu juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na mazingira,
tatueni kero za wananchi, toeni taarifa za mapokezi ya fedha za serikali pia
mkaongeze bidii katika kukusanya wamapato ya serikali katika maeneo yenu,"
alisema Mhe. Mndeme.
Katika hatua nyingine Mhe. Mndeme amewaeleza
wataalam hao kuwa serikali ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta zaidi
ya Trilioni moja fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika
sekta mbalimbali huku akiwataka kwenda kuzisimamia ili zililete matokeo chanya
kwa wananchi katika maeneo yao
Aidha amewataka wakurugenzi wa halmashauri
zote za mkoa huu kuhakikisha wanalipa stahiki za watumishi wao, kuandaa mafunzo
ya watumishi, kutatua kero za wananchi na watumishi katika halmashauri zao ili
wamsaidie Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na ndiyo maelekezo yake huku akiwataka kuchapa kazi kwa bidiii zaidi
Kwa upande wao wakurugenzi wa halmashauri hizi
za mkoa wa shinyanga wamekiri kupokea maelekezo ya Mhe. Mndeme na kumuahidi
kuwa wanakwenda kuyatekeleza maelekezo yote ikiwemo utatuzi wa migogoro na
kulipa stahiki za watumishi wao.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mwl.Kagunze akizungumza katika kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Profesa Siza Tumbo akizungumza katika kikao kazi
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akizungumza katika kikao kazi.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akizungumza katika kikao kazi.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mwl.Kagunze akizungumza katika kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakiwa kwenye kikao kazi.
Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wakichangia mawazo yao kwenye kikao kazi.
0 Comments