6/recent/ticker-posts

TIMU 16 KUSHIRIKI LIGI YA JAMUKAYA RAMADHAN CUP 2024 KATIKA DIMBA LA SHY COM SHINYANGA


Meneja Rasilimali Watu, Utawala na Sheria wa Kampuni ya Jambo Group, Wakili John Palamagamba Kabudi akizungumza na Vyombo vya Habari leo Jumatano Machi 6,2024

Meneja Rasilimali Watu, Utawala na Sheria wa Kampuni ya Jambo Group, Wakili John Palamagamba Kabudi akizungumza na Vyombo vya Habari leo Jumatano Machi 6,2024

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Michuano ya Jamukaya Ramadhan Cup msimu wa 2024 inatarajia kuanza kutimua vumbi ukatika uwanja wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (Shycom) Mjini Shinyanga kwa timu 16 kuwania ubingwa wa michuano hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jumatano Machi 6,2024 Meneja Rasilimali Watu, Utawala na Sheria wa Kampuni ya Jambo Group, amesema Michuano hiyo itaanza kutimua vumbi kuanzia tarehe Machi 14, 2024 hadi Aprili 3,2024.

Ameeleza kuwa michezo itakuwa inafanyika kuanzia saa 3:00 usiku na kwamba lengo la mashindano hayo ni kusaidia watu wenye uhitaji wakiwemo wajane na watoto yatima.


"Ligi hii ya Jamukaya Radhaman Cup itafanyika katika kipindi cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na itakuwa ligi ya mtoano dhumuni kubwa ni kusaidia watoto yatima na wajane. Maandalizi ya kufunga taa uwanjani yanaendelea. Mwisho wa kuchukua fomu za kushiriki michuano hii ni Machi 11,2024 ambapo siku hiyo pia tutatangaza zawadi zitakazotolewa kwa washindi katika kinyang'anyiro hicho",amesema Wakili John

Post a Comment

0 Comments