6/recent/ticker-posts

BARAZA LA UWT SHINYANGA LA KETI MWENYEKITI AKEMEA WAPIGA MAJUNGU ,AHAMASISHA UJENZI WA NYUMBA YA KATIBU WA UWT


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake UWT mkoa wa Shinyanga Grace Bizulu akizungumza na wajumbe wa baraza la UWT Mkoa .

Na Suzy Luhende

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake UWT mkoa wa Shinyanga Grace Bizulu amewataka wanachama wa UWT kishikamana ili kukijenga chama kuliko kuendelea kutendengeneza makundi na kupiga majungu hali ambayo inaweza kukigawa chama hicho na kusababisha mpasuko mkubwa ndani ya jumuiya na CCM.


Grace amesema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga, lililofanyika katika ukumbi mdogo wa CCM mkoa, ambapo amesema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitengene
za makundi na kuwasema viongozi waliopewa dhamana ya kukiongoza chama hicho , hali ambayo imekuwa ikisababisha mpasuko mkubwa kwa wabunge na wanachama.


Grace amesema kuwa uchaguzi umeisha, kila mmoja afanye majukumu yake ya kazi haitakiwi tena kupigana mikumbo, ifikie sehemu kila mmoja ampende mwenzake na kuweza kukisemea vizuri chama cha mapinduzi na kusikiliza kero zilizopo kwenye jamii na kuzitatua kwa sababu wote ni watoto wa mama mmoja CCM na tunasimamia ilani ya Chama.

"Imefikia wakati tunaanza kurekodiana mmezidi hiyo tabia niwaombe muache mara moja, nikimjua mtu anayechonanisha nitamwambia katibu asimualikie kwenye vikao vyangu, tuweni na hofu ya Mungu tupendane pale tunapokosea tuambizane tusiendekeze majungu hayajengi yanabomoa,"amesema Mwenyekiti Bizulu.

"Niwaombe ndugu zangu tuwe na upendo na mshikamano tusiwe wabomoaji wanaopenda kuvuruga na kujipendekeza, kwani watu wanaofanya hivyo wanatuharibia mkoa wetu na kuonekana hatuna ushirikiano na umoja, ndiyo maana tunashindwa kupata wageni wakubwa kwa sababu ya watu wachache wanaopenda kujipendekeza, amesema Bizulu.

"Sisi kina mama tunatakiwa tuwe na upendo na mshikamano,tufanye kazi kama tulivyoahidi wakati tunaomba kura kwa wananchi, niombe huu wakati mniache nifanye kazi, kwa kushirikiana na wabunge wangu wote, sitaki mambo ya ubaguzi tusibaguane kwamba huyu ni wa nani na huyu ni wanani tufanye kazi kwa pamoja, wale waomba fedha watafute njia zingine za kushawishi sio kusema uongo," ameongeza Bizulu.

Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Shinyanga Rucy Mayenga  amewaomba wanawake kutoa ushirikiano ili kuhakikisha wanajenga nyumba ya katibu wa UWT na ofisi ya wabunge kwani wabunge hawapo nyuma katika kufanya maendeleo ambapo amechangia shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga nyumba hiyo huku 
Santiel Kilumba akichangia shilingi milioni 6 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo..


Kwa upande wake Katibu wa UWT mkoa wa Shinyanga Asha Kitandala akiwa na wajumbe wa baraza wametembelea eneo la ujen
zi na kukagua ujenzi wa nyumba ya katibu wa UWT mkoa inayojengwa katika maeneo ya Bushushu kata ya Lubaga ambapo ameeleza kuwa tayari wameanza ujenzi ambao utachukua siku 16 kufikia tarehe 12, 8, 2023 , ambapo pia katika eneo hilo watajenga vibanda nane kwa ajili ya biashara.

Kwa upande wake mjumbe wa baraza la UWT Taifa Christina Gule amewaomba wanawake kuendelea kuwa na ushirikiano ili waweze kufanya mambo makubwa ndani ya CCM waendelee kutatua kero mbalimbali, wakishirikiana na wabunge,katika kuinua maendeleo ya jumuiya na chama.

"Wabunge wetu tunawapenda sana karibuni sana mjisikie vizuri kinachotakiwa ni kuwa na ushirikiano, sasa mkoa wetu umetulia tuendelee kumuomba Mungu aendelee kutusimamia ili tuweze kufanya mambo makubwa ndani ya CCM, tuendelee kutatua kero mbalimbali wabunge wetu njooni tufanye kazi ya UWT kina mama tupo kwa ajili ya kufanya kazi,amesema Gule

"Ni heshima kubwa kuanzisha ujenzi huu, kwani toka ianzishwe UWT mkoa wa Shinyanga haijawahi kujengwa nyumba ya katibu wa UWT, na sasa tunaendelea kujenga tunawashukuru chama mkoa kwa kuendelea kutusapoti na tunawashukuru wabunge wetu kwa kuendele kutushika mkono tumeanza leo kujenga, niwaombe wajumbe wa baraza tuendelee kutafuta fedha ili nyumba hii imalizike kwa wakati,"amesema Gule.

Kikao cha baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga kimefanyika leo katika ukumbi mdogo wa CCM Mkoa, ambapo pia wajumbe wa baraza hilo waliambatana na mbunge viti maalumu Santel Kilumba kwa ajili ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya katibu katika maeneo ya Bushushu manispaa ya Shinyanga.

Mbunge viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Lucy Mayenga akizungumza kwenye baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga
Mbunge viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Lucy Mayenga akizungumza kwenye baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga nakuahidi kutoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya ujenzi wanyumba ya katibu wa UWT mkoa.
Mbunge viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Santiel Kilumba akizungumza kwenye baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga na kuahidi kuchangia shilingi milioni 6 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya katibu wa UWT.
Mbunge viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Santiel Kilumba akizungumza kwenye baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga .
Wajumbe wa baraza la UWT Mkoa wa Shinyanga wakiendelea na kikao.


Katibu wa UWT wilaya ya Shinyanga  Sharifa Hassan Mdee akizungumza kwenye kikao cha baraza mkoa wa Shinyanga
Katibu wa UWT wilaya ya Shinyanga  Sharifa Hassan Mdee akizungumza kwenye kikao cha baraza mkoa wa Shinyanga











































































































Post a Comment

0 Comments