Katibu Tawala Mkoa wa
Shinyanga Pro. Siza D. Tumbo amefunnga kambi ya michezo na kuwatakia ushindi
timu ya UMITASHUMTA mkoa wa Shinyanga katika mashindano yao Kitaifa wanayokwenda
kushiriki katika Manispaa ya Tabora Mkoa wa Tabora.
Pro. Siza ameyasema
hayo leo tarehe 1 Juni, 2023 wakati wa alipokuwa akizungumza na timu ya
wanamichezo wa UMITASHUMTA katika ukumbi wa mikutano uliopo Chuo cha Ualimu
Shinyanga (SHYCOM) huku akisisitiza kuwa ili warudi na ushindi wanapaswa
washindane kwa umakini, bidii, maarifa na nidhamu wakati wote watakapokuwa
katika mashindano hayo.
“Rai yangu kwenu
wanangu, wanamichezo na wawakilishi wa Mkoa wetu kwenda kushindana kwa bidi,
maarifa na nidhamu kubwa wakati wote huku mkizingatia kuwa Mkoa umewaamini na
ndiyo maana kati ya wengi mmechaguliwa ninyi kutuwakilisha, na katika hili
niseme tu kwamba Serikali ya Mkoa wa Shinyanga ipo nanyi wakati wote na mimi
binafsi ni muumini wa michezo kwakuwa najuwa michezo ni zaidi ya burudani,
michezo ni afya, ni undug una kikubwa michezo ni ajira kama zilivyo ajira
nyingine,” alisema Pro. Siza.
Pro. Siza alitumia
fulsa hiyo kuwaeleza walimu katika shule zote Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha
kuwa wanakuwa na vipaumbele vya michezo katika shule zao zote za Msingi na
Sekondari kama ambavyo imeoneshwa kwenye program ya uendeshaji wa michezo na
utamaduni ambayo inaonesha kila siku kutakuwa na muda maalumu kwa ajili ya
michezo, sanaa na utamaduni huku akiwataka kupanda mbegu za michezo za muda
mrefu ili baada ya miaka mitano ijayo Shinyanga iwe ya mfano.
Akisoma taarifa ya
mashindano ya michezo Mkoa wa Shinyanga kwa mwaka 2023 Mwalimu Mayasa
Mwinyijuma alisema kuwa, kambi ya UMITASHUMTA 2023 Mkoa wa Shinyanga ilianza
mara baada ya mashindano ya Halmashauri kukamilika tarehe 22 Mei, 2023 ambapo
alizea kabla ya ngazi ya Mkoa mashindano hayo yalifanyika ngazi ya shule, kata,
kanda na Wilaya ili kupata timu za Wilaya.
Timu ya UMITASHUMTA MKoa wa Shinyanga imeondoka kuelekea Manispaa ya Tabora Mkoani Tabora na wanafunzi 120, walimu wa michezo 14 na daktari wa michezo 1.
Burudani zinaendelea katika ukumbi wa chuo cha Ualimu Shinyanga .
0 Comments