6/recent/ticker-posts

HALMASHAURI YA SHINYANGA YAPATA HATI SAFI ,RC MNDEME AWAPA MTIHANI MZITO MADIWANI NA WATAALAMU


mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme kwenye kikao maalum cha Baraza la Madiwani.
 NA AMO BLOG SHINYANGA.

Serikali mkoani Shinyanga imeuagiza uongozi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga mkoani humo kuhakikisha wanaongeza juhudi za ukusanyaji mapato ili waweze kufikia malengo waliyo jiwekea ya kukusanya mapato kwa asilimia 100 .

Maagizo hayo yametolewa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme kwenye kikao maalum cha Baraza la Madiwani walicho keti kwa ajili ya kupokea ,kupitia na kujadili hoja ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG

Mndeme amebainisha kuwa kuanzia mwezi Julai 2022 hadi  Juni 19, 2023 wamefikia asilimia 75 ya ukusanyaji wa mapato na kueleza kuwa kisi cha asilimia 25 bado kinahitajika ili kufikia malengo waliyojiwekea katika ukusanyaji mapato kwa mwaka.

Aidha Mndeme ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa kupata hati safi huku akiwasii kudumisha umoja namshikamano baina ya wataalamu na madiwani hali itakayo saidia kuongeza kiwango cha ukusanyaji wamapato na kuchochea maendeleo ya halmashauri hiyo.

Halmashauri hii inatakiwa isimamie sheria,kanuni na miongozo kwani nafahamu mnaweza maana mnayo timu nzuri ya wataalamu na madiwani ambao wamesababisha halmashauri kupata hati safi” amesema Mndeme.

Awali mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Simon Barege akizungumza katika kikao hicho ameahidi kutoa ushirikiano kwa madiwani na kutumia maarifa aliyo nayo kuchochea maendeleo ya halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Naye Mkaguzi Mkuu wa Hsabau za Serikali Mkoa wa Shinyanga, Patrick Lugisi ameshauri kamati ya fedha kuandaa taarifa za muhtasari wa kikao vizuri ili kurahisisha kazi kwa wakaguzi na kufanikiwa kujibu hoja.

“Halmashauri hii inahoja 56 ambazo bado hazijajibiwa zinatakiwa kufanyiwa kazi ili isibaki hata hoja moja , amesema Lugisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje ameahidi kushirikiana na madiwanipamoja na wataalamu kutekeleza maagizo yaliyo tolewa na mkuu wa mkoa.


Mwenyekiti wahalmashauli ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje katikati akiendesha kikao.

mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Simon Barege

Maombi ya kuiombea halmashauri yanaendelea.

Mambo ya ufunguzi wa kikao cha baraza maalumu la madiwani yanaendelea.


Maombi yanaendelea.


mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Simon Barege akizungumza katika baraza maalumu la madiwani.



Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Prf.Siza Tumbo akiwa kwenye kikao cha baraza maalumu la madiwani.



Mwenyekiti wahalmashauli ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje katikati akiendesha kikao.





Madiwani wakiwa kwenye kikao cha baraza maalumu la madiwani.






mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Simon Barege.

Post a Comment

0 Comments