6/recent/ticker-posts

TAJOGEV YA WAPA MBINU ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA WAANDISHI WA HABARI KUTOKA MIKOA TISA


Na Marco Maduhu, SHINYANGA

MTANDAO wa Waandishi wa Habari wa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia Tanzania(TAJOGEV)umetoa elimu ya kuwajengea uwezo na uelewa wa pamoja waandishi wa habari kutoka mikoa tisa hapa nchini, katika kuendeleza mapambano ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.

Mafunzo hayo yametolewa leo Julai 13, 2023 Mkoani Shinyanga na yatahitimishwa kesho, huku Mgeni Rasmi akiwa ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Johari Samizi.

Mwezeshaji Deogratius Temba akitoa mafunzo.
Mwenyekiti wa (TAJOGEV) Stella Ibengwe.

Mwenyekiti wa Mtandao wa waandishi wa habari za kupambana na ukatili Tanzania (TAJOGEV) Stella Ibengwe, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, amesema lengo la kuanzisha Mtandao huo, ni kupaza sauti juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, na mpaka sasa Mtandao umeshafikisha wanachama 96 kutoka mikoa 10.
Amesema wamewaita waandishi wa habari kutoka mikoa tisa, ambayo ni Mwanza, Mara, Kagera, Kigoma, Geita, Singida, Tabora, Simiyu na wenyeji Shinyanga, kwa ajili ya kuwajengea uwezo na uelewa wa pamoja katika masuala ya ukatili wa kijinsia kwa kuongeza nguvu ya pamoja kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.



















Post a Comment

0 Comments