6/recent/ticker-posts

MAHAFALI YA 3 YA WANAFUNZI WA AWALI SHULE YA AWALI NA MSINGI SAPPS YA FANA SHINYANGA ,WAZAZI WAOMBWA KUWEKEZA SEKTA YA ELIMU

Wahitimu wa darasa la awali SAPPS wakikabidhiwa vyeti na mgeni rasimi.

Na Amo Blog Shinyanga. 

Wahitimu wa Awali wanao soma Shule ya Shinyanga Adventist Pre and Primary School (SAPPS) Inayo milikiwa na Nyanza Gold Belt Field  (NGBF) yenye usajili wanamba EM18166 wamehitimu mafunzo yao ya awali ikiwa ni mandalizi ya kujiunga na masomo ya darasa la kwanza mwaka 2024.

 Akizungumza na wazazi na walezi wawatoto walio hitimu mgeni rasmi katika mahafali hayo Kiliani Wembe amewataka kuwaandikisha elimu ya msingi watoto wote waliohitimu elimu ya awali ili waweze kuanza darasa la kweanza mwakani.

 Pia Wembe ametoa kiasi cha shilingi laki tano ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za shule hiyo katika kuboresha miundo mbinu ya shule hiyo huku akiahidi kulipa gharama za fomu kwa wazazi na walezi watakao jitiokeza kuandikisha watoto wa nao anza darasa la awali mwaka 2024.

 Aidha wembe ameipongeza shule hiyo kwa kufanya vizuri kitaaluma ikiwemo kusisitiza nidhamu na maadili kwa wanafunzi wanao soma katika Shule hiyo.

 Naye Mwalimu mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Elijali Waritu amesema kuwa shule hiyo imejipanga kuendelea kutoa elimu bora na kufanya vizuri kitaaluma huku akiwaomba wazazi na walezi kujenga utamaduni yakutembelea shule hiyo ili waweze kuona maendeleo ya watoto wao. 

Wahitimu wa darasa la awali SAPPS wakiwa kwenye picha ya pamoja .

Wahitimu wa darasa la awali SAPPS wakionyesha burusani.

Wahitimu wa darasa la awali SAPPS wakitoa burudani.

Wahitimu wa darasa la awali SAPPS wakiwa kwenye mahafali.





















Post a Comment

0 Comments