6/recent/ticker-posts

ASKOFU BUGOTA AONGOZA MAADHIMISHO YA JUMUIYA YA UMOJA WA MAKANISA YA KIKRISTO(CCT ) MANISPAA YA SHINYANGA ,ASISITIZA WAKRISTO KUOMBEA UCHAGUZI

Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga Askofu Zakayo Bugota , akiongoza maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .

Na Amo Blog Shinyanga.

Leo, Machi 7, 2025, Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga Askofu Zakayo Bugota , ameongoza maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga mkoani humo.

 Maadhimisho hayo yamefanyika katika Kanisa la Mennonite Ngokolo na kuhudhuriwa na waumini kutoka katka makanisa mbalimbali ya CCT katika Manispaa hiyo.

Katika maadhimisho hayo, Askofu Bugota amesisitiza umuhimu wa wakristo kudumisha umoja wa CCT na kupongeza jitihada za wanajumuiya wa makanisa ya Kikristo katika kutoa huduma za kitume na kijamii kwa jamii.

Bugota amewataka wana CCT kuwa na roho ya mshikamano, upendo, na kutoa msaada kwa wengine kwa kusaidia jamii,kwa kutoa huduma za kijamii na za kiroho, ili kuhakikisha ustawi wa jamii nzima.

Askofu Bugota ametoa wito kwa waumini kuendelea kuliombea taifa la Tanzania katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu kwani ni muhimu kwa waumini wote kuwa na sala za dhati kwa ajili ya amani ya taifa letu, na kwamba watanzania wanapaswa kushirikiana na kudumisha umoja kwa manufaa ya Taifa.

Neno la Mungu lililoongoza maadhimisho hayo limetoka kitabu cha Zaburi 139:14, ambalo linasema: "Nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu." Neno hili linalenga kuwakumbusha waumini kuwa kila mtu ameumbwa kwa mpango wa kipekee na wa ajabu kutoka kwa Mungu, na hivyo kila mmoja anapaswa kuthaminiwa na kuthamini utu wake.

Maadhimisho haya yalileta faraja na msukumo kwa waumini wengi, na kwa pamoja walijitolea kuombea taifa letu, familia zao, na makanisa yao ili iwe na maendeleo endelevu na Amani.

Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga Askofu akayo Bugota , akishiriki maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga Askofu akayo Bugota , akiwa kwenye maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Mwinjiristi kutoka kanisa la mtakatifu Andrea kitangili Alisia Christopher akitoa mahubili kwa waumini walioshiriki maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kumsikiliza askofu Bugota katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kumsikiliza askofu Bugota katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga.
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Viongozi wa dini wakiwa maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .
Waumini wakiendelea kusifu na kuabudu katika maadhimisho ya Jumuiya ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo (CCT) Manispaa ya Shinyanga .

Tazama picha wakati maadhimisho yakiendelea.





































Post a Comment

0 Comments