6/recent/ticker-posts

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA YAMPONGEZA DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUTIMIZA MIAKA MI 4 MADARAKANI

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mhamasishaji mkubwa wa ulipaji kodi nchini. 
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Bw.Yusuph Juma Mwenda akimpongeza Dkt.Samia kwa kazi kubwa ya kuhamasisha ulipaji kodi.

Pongezi hizo zimetolewa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Bw.Yusuph Juma Mwenda, ambaye ameonyesha kuridhishwa na juhudi za Rais Samia katika kukuza utamaduni wa ulipaji kodi.

Kamishna Mwenda mbali na kumpongeza Dkt.Samia pia amesisitiza umuhimu wa kila raia na mfanyabiashara kutimiza wajibu wake wa kulipa kodi kwa hiari, huku akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa na ustawi wa wananchi.

Aidha, Kamishna Mkuu amekemea vikali vitendo vya ukwepaji kodi na kusema kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania itaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya watu wote wanaoshiriki vitendo vya kukwepa kulipa kodi, ili kulinda maslahi ya nchi na kuhakikisha maendeleo endelevu.

TRA inaendelea kufanya juhudi za kuhamasisha wananchi na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa ulipaji kodi ili kuhakikisha kuwa rasilimali za taifa zinatumika vizuri kwa ajili ya maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments