6/recent/ticker-posts

MBUNGE JIMBO LA SOLWA, MHE. AHMED SALUM AENDELEA NA ZIARA YAKE ,CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KATA YA MWAKITOLYO WAMKABIDHI CHETI CHA PONGEZI

Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum Akipokea cheti cha pongezi kutoka kwa vuongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutokana na juhudi zake kubwa katika kupigania maendeleo ya wananchi 

Na Amoj Media Shinyanga.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga mkoani humo kimemtunuku cheti cha pongezi Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum, kutokana na juhudi zake kubwa katika kupigania maendeleo ya wananchi wa kata hiyo na jimbo la Solwa kwa ujumla.

Zoezi la kumkabidhi cheti cha pongezi Mhe.Mbunge limefanyika Machi 21,2025, katika kata hiyo, wakati wa ziara ya Mhe. Ahmed Ally Salum ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza kero zinazo wakabili wananchi wa kata hiyo.

Katika ziara hiyo Mhe.Ahmed ametembelea kijiji cha Nyang'ombe na kukagua ujenzi wa zahanati yenye thamani ya shilingi 91,600,000/=ambayo imejengwa kupitia ufadhili wa wadau mbalimbali na serikali na kuaahidi kutoa shilingi 2,000,000/= kwa ajili ya kukamilisha mfumo wa maji katika zahanati hiyo ili kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wagonjwa na wahudumu wa afya wanao fanya kazi katika zahanati.

Aidha Mhe. Ahmed amewashukuru wadau waliochangia ujenzi wa zahanati hiyo, akisema kuwa imesaidia kupunguza adha ya wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za matibabu. na kuwaomba wadau kuendelea na moyo huo wa kujitolea katika kuchangia miradi ya maendeleo.

Pia, Mhe. Ahmed alifanya ziara katika Kata ya Solwa, Kijiji cha Manheigana, na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Manheigana. Aliahidi kuchangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule hiyo. Aidha, alitoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kujifungulia akina mama katika Kata ya Solwa, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha miundombinu ya sekta ya afya nchini.Wananchi wakimshangilia mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum alipowasili katika kata hiyo kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi.

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wakimkabidhi cheti cha pongezi Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum kutokana na juhudi zake kubwa katika kupigania maendeleo ya wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum Akipokea cheti cha pongezi kutoka kwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutokana na juhudi zake kubwa katika kupigania maendeleo ya wananchi 
Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum Akipokea cheti cha pongezi kutoka kwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutokana na juhudi zake kubwa katika kupigania maendeleo ya wananchi 
Mbunge Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum akiwashukuru wananchi.
Mbunge Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum akisikiliza kero za wananchi.
Wananchi wakimsikiliza mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum wakati akisikiliza kero za wananchi.
Wananchi wakimsikiliza mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Ally Salum wakati akisikiliza kero za wananchi.

TAZAMA PICHA  MATUKIO YA ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA SOLWA, MHE. AHMED IKIENDELEA .


















 

Post a Comment

0 Comments