6/recent/ticker-posts

SHIRIKA LA MHOLA LA TOA MBINU ZA WANAWAKE KUWA VIONGOZI MULEBA MKOANI KAGERA.


Mkurugenzi wa shirika la Mhola  Bwana Saulo Marauli akizungumza na washiriki wa semina.

Na Mwandishi wetu Amo blog Muleba.

Shirika lisilo la Kiserikali linatoa msaada wa Kisheria Mhola limetoa elimu ya kushiriki kwenye fulsa za uongozi kwa kina mama  Wilayani Muleba Mkoani Kagera ambao utawasaidia kushiriki kwenye vikao vya maamuzi pamoja na kuonesha uwezo wao wa uongozi.

Akifungua mafunzo hayo mkurugenzi wa Shirika la Mhola Bwana Saulo Marauli amesema mafunzo hayo yanahusisha Wanawake Viongozi  wa Serikali za vijiji kutoka Kata za Katoke, Izigo na Muhutwe ambayo yatafanyika kwa muda siku mbili kwenye ukumbi wa makao makuu ya shirika hilo Wilayani Muleba.

Bwana Marauli amesema kuwa bado kwenye jamii kuna changamoto ya baadhi ya wakina mama kushindwa kujiuhusisha na shughuli za kiuchumi ikiwemo kufuga na kulima badala yake wanakuwa tegemezi kwenye jamii hivyo mafunzo hayo yatawasaidia wakina mama kujua haki zao ikiwemo sheria, uchumi na afya zao.

 Wakili Raymond Laurent kutoka Shirika la Mhola amewataka wakina mama kuwa na mawazo chanya ambayo yatawasaidia kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa lengo la kujikwamua kiuchumi badala ya kubaki kuwa tegemezi kwenye jamii.

Wakili Laurent amesema kuwa wanawake viongozi wanaowajibu wa kuhakikisha wanakuwa mfano bora wa kuigwa kwenye jamii ikiwemo kuondoa upendeleo, kusuruhisha, kuacha alama na kuinua kiwango cha utendaji kazi kwa lengo la kuendelea kuaminiwa na jamii.

 Aneth John ni Mtendaji wa Kijiji cha Kimbugu na Alikanjera Audax ni mwenyekiti wa Kitongoji cha Bulimba wamesema kuwa bado wakina mama wamekuwa na changamoto ya kunyanganywa mali zao ikiwemo mashamba na nyumba na kubaki tegemezi baada ya kukopeshwa na taasisi za kifedha na kushindwa kurejesha kutokana na uhaba wa elimu ya matumizi sahihi ya fedha hivyo kuna haja ya kupatiwa elimu ili kuondoa changamoto hiyo.

Aidha shirika hilo la Mhola linatarajia kutoa mafunzo kwa Wanawake Viongozi kwa mwaka 2023 kwenye Kata ambazo ni Izigo, Kasharunga, Katoke, Muhutwe, Mubunda, Kagoma, Bureza na Gwanseri na Kijiji cha Kyamworwa lengo ni kuhakikisha wakina mama hao wanatumia fulsa za kiuchumi zilizopo kwenye maeneo yao.

Wakili Raymond Laurian akitoa elimu ya uongozi kwa washiriki wa semina hiyo




WaShiriki wakisikiliza kwa mada mbalimbali zinazofundishwa kutoka kwa wawezeshaji.


Mtendaji wa Kijiji Cha Kimbugu akichangia mawazo juu ya mada ya wanawake na uongozi




 

Post a Comment

0 Comments