6/recent/ticker-posts

MENEJA TRA SHINYANGA MARO AWAKUMBUSHA WAFANYABIASAHARA AMBAO BADO AWAJA FANYA MAKADILIO KUFIKA OFISINI KABLA YA MACHI 31


Na Amoj Media Shinyanga.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Shinyanga, Emmanuel Maro amewakumbusha wafanyabiashara mkoani Shinyanga ambao bado hawajafanya makadilio ya kodi kufika TRA na kufanya makadilio yakodi yao katika kipindi hiki cha Malipo ya kodi kwa awamu ya kwanza kabla ya Tarehe 31 mwezi Mach mwaka huu.

Maro Mbali na kuwahimiza wafanyabiashara kufanya makadilio na kulipa kodi yao ya awamu ya kwanza pia amewahimiza wafanyabiashara kutunza kumbukumbu za manunuzi na matumizi ya mashine za EFDs (Electronic Fiscal Devices) ili kuboresha uwazi na ufanisi katika ulipaji wa kodi. 

Amesema kuwa matumizi ya EFDs ni muhimu kwa kuhakikisha kila muamala unarekodiwa na kodi inalipwa ipasavyo.

Aidha Maro amewashukuru Wafanyabiashara wa mkoa wa Shinyanga kwa kutoa ushirikiano kwa Mamlaka hiyo kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari kwani kufanya hivyo ni kuimarisha uchumi wa mkoa na Taifa kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments